Geric FM

PESA SIO MALIGHAFI!




Gazeti la DJ na: Gerald Joseph/DjGeric
Pesa ni kitu kilichopewa thamani na kikapewa uwezo wa kutumika katika hali tofauti hasa ile hali ya kubadilishana na vitu vingine yaani kununua au kuuza vitu. Ila sasa…

Pesa hii ambayo ipo katika muundo wa noti na sarafu sio marighafi ya kuzalisha hivyo vitu vingine ambavyo inabadilishana navyo, mfano magari, vyakula, nguo, mafuta nakadhalika. Kiasi kwamba hata bila pesa vitu hivyo vingeweza kuwafikia watu kama ilivyo sasa.
Mfano; wanaosafirisha bidhaa kwenye vyombo mbalimbali hawatumii pesa kubeba hizo bidhaa, wanaozalisha mafuta hawatumii pesa kutengeneza mafuta hayo au wanaotengeneza nguo hutumia vitu vingine na sio pesa

UTAMU WA PESA
Pesa imekuwa tamu kiasi kwamba hata watu wameitukuza kuliko kitu kingine chochote. Imefika mahali watu wanafanya mambo ya kuwateketeza ndugu na jamaa zao kwa sababu ya kuitafuta pesa.
Pia imekuwa vigumu sana kupata mahitaji ya kumwezesha mtu kuishi bila pesa, mambo kama chakula, mavazi na malazi na hata vinginevyo. Lakini pia mambo ya starehe nayo bila pesa ni vigumu sana kuhusika nayo zaidi ya kubaki kuyasikia tu masikioni mwa watu wengine. Jambo linguine na nyeti sana ni swala la afya ambapo kuna hospitali mtu hapati huduma kabla ya kuonesha kadi ya malipo hata kama ana hali gani, hivi vyote na vingine ambavyo sijataja hapa ni kuonesha namna gani pesa inapendwa na karibia kila mtu alihali pesa hii sio marighafi.

MAONI YA MHARIRI
Lengo na dhumuni la gazeti hili la dj sio kushusha thamani ya pesa ya nchi au mtu yeyote au kuwasema waliotengeneza pesa bali ni kuonesha namna ilivyopewa sana kipaumbele kuliko hata maisha ya mtu, kwa sababu wako watu ambao wanadiriki hata kuwaua wazazi au watoto wao au mtu yeyoye ili wapate hio pesa ambayo sio marighafi.
Pia lengo la gazati hili ni kuwahimiza watu au jamii kukemea njia zote mbaya zinazotumika kuitukuza pesa kuliko uhai wa mtu.

Imetolewa Na,
Gerald Joseph/DjGeric
kwa maoni tuandikie kutumia barua pepe: gericfm@gmail.com
PESA SIO MALIGHAFI! PESA SIO MALIGHAFI! Reviewed by GericFM on June 21, 2017 Rating: 5

No comments:

Vistros

Powered by Blogger.