Geric FM

ETI KUJIONGEZA!



GAZETI LA DJ
ETI  KUJIONGEZA!
Katika maisha ya wanadamu kumekuwa na ile hali ya kuboresha maisha kwa kutafuta chakula, mavazi, nyumba nzuri, elimu na kadhalika. Lakini maisha haya pamoja na hivyo vyote vinavyotafutwa vimetawaliwa sana na pesa.

Kwa maana kuwa bila pesa inakuwa vigumu kuvipata vitu hivyo. Pia njia za kupata pesa zimekuwa zikiwatatiza walio wengi sana na pia kumekuwa na wengi wanaoshauri au kuhamasisha wenzao KUJIONGEZA.

 
 Wakimanisha kuwa watafute njia za kupata pesa ili kuweza kuyaboresha maisha yao, ni vizuri sana kabisa kuelezana njia za kuishi vizuri ila tatizo ni pale wengi walipolalia upande mmoja katika dhana hio ya kuiongeza, na upande huo ni wa biashara.

Hapa sio kila mtu anawea kufanya biashara kama wanavyohamasisha baadhi ya watu. Na dhana hii ya kufanya biashara inatokana na dhana nyingine ya ajira/kujiajiri.
Katika dhana hii ya kujiajiri ni kwamba sio kila mtu pia anaweza kujiajiri licha ya kuwa na uwezo fulani kama vile pesa na rasilimali zingine.
Hivyo kuwa na matabaka ya wajiriwa na waajiri, nah ii ni kutokana na utofauti tulionao wanadamu katika kuwaza na kuamua mambo katika maisha yetu.
Hivyo basi neon linalotumika kwa kuwahimiza watu kutafuta njia za kupata pea na wengi wakimanisha kujiajiri kuna watu linawafaa na kuna watu haliwafai wala kuwasadia kwa sababu kuna watu wao wako hivyo yani aidha waajiriwe au watunzwe ili kuboresha maisha yao katika kuhakikisha wanapata mahitaji muhimu na za ziada.

MAONI YA MHARIRI
Kabla ya kujiongeza angalia uwezo wako katika swala zima la kuboresha maisha uliyonayo au kutimiza mahitaji yako muhimu nay a ziada. Neno KUJIONGEZA lenye maana ya kujiajiri au kufanya biashara kama wengi wanavyolitumia lisikufunge na kukufanya ukafanya usiloweza eti kisa ndo wengi wanasema kinafaa.
Pia nia na lengo la Gazeti la Dj sio kukinzana na wote wanahamashisha jitahada mbalimbali za kuwaweza wengine kujikwamua na kuyaboresha maisha yao bali ni kuonesha utofauti tulionao wanadamu pia kushauri zitafutwe mbinu zingine za kuwasaidia wasioweza kujiongeza kwa kufanya biashara au kwa kujiajiri.

Imetolewa na kuandikwa na:
Gerald Joseph/DjGeric
WhatsApp namba: +255689 492 656
ETI KUJIONGEZA! ETI  KUJIONGEZA! Reviewed by GericFM on June 06, 2017 Rating: 5

No comments:

Vistros

Powered by Blogger.